The House of Favourite Newspapers

Fifa Yamfungia Kiungo Mpya Yanga

Kiungo Mzan­zibar, Mohammed Issa ‘Banka’.

KUNA picha ambalo mashabiki wa Yanga walikuwa wanakuna vi­chwa kwa vile walikuwa hawaelewi linaendaje. Lile la Kiungo wao Mzan­zibar, Mohammed Issa ‘Banka’ waliyemsajili kwa gharama kutoka Mtibwa.

 

Ukweli ni kwamba Banka amesimamishwa au kufun­giwa kucheza soka kwa miezi mitatu.

Adhabu hiyo imetolewa na Shirikisho la Soka la Ki­mataifa (Fifa) ambalo lilibaini Banka kutumia madawa ya­nayoongeza nguvu ambayo hayakubaliki michezoni.

 

Kutokana na hali hiyo, Fifa imeamua Banka kutocheza kwa miezi mitatu na atakuwa chini ya uangalizi wake. Baada ya hapo, wataalamu wake watatua nchini ku­chukua vipimo tena ili kupata uhakika kama anatumia au la.

 

Habari za uhakika kutoka jijini Zurich zimeeleza, Banka amefungiwa baada ya ku­bainika alitumia kilevi hicho kwa zaidi ya asilimia 150.

“Alitumia kilevi hicho kwa zai­di ya asilimia 150, nafikiri ilifika 200 na kitu. Lakini Fifa wana­muona bado mdogo, wametoa nafasi ya miezi mitatu. Maana wakati wa kumhoji alitoa ushiri­kiano kwa asilimia kubwa sana, wakaona wampe nafasi ya kujirekebisha,” kilieleza chanzo cha uhakika.

 

“Viongozi wa soka hapo wamekuwa wakificha, lakini TFF wanajua muda mrefu. Huenda walifanya hivyo kulinda maadili kutokana na kazi yao. Yanga pia wanajua, wamekuwa wak­ificha tu,” kilisisitiza chanzo.

 

Banka alipimwa wakati wa michuano ya Kombe la Cha­lenji, Kenya wakati Zanzibar ilipotinga fainali ya michuano hiyo na kufungwa na wenyeji.

Taarifa nyingine zinasema baada ya Banka kung’ara wakati Taifa Stars ikiitwanga DR Congo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ndipo wataalamu hao wa Fifa walipo­jiridhisha kuhusiana naye na kubaini kweli alikuwa akitumia kilevi hicho.

 

Kwa mujibu wa sheria za Fifa, anayebainika anatumia madawa kwa kiwango zaidi ya asilimia 150, hufungiwa hadi miaka minne lakini chanzo kingine kutoka jijini Nairobi ambako yalichukuliwa majibu hayo kimesema:

 

“Kwa huyo kijana wenu akifungiwa labda miaka miwili. Fifa waliona ame­wapa ushirikiano lakini wanamchukulia kama kijana anayekua. Lakini wakiona ameacha kabisa, basi atasal­imika.”

 

Yanga walimng’oa mche­zaji huyo mikononi mwa Simba na Singida United ambazo nazo zilikuwa zikim­mezea mate, lakini Cham­pioni Jumatano hatimaye limebaini ukweli baada ya kufanya uc hunguzi wa kina ndani ya Yanga pamoja na kwa maswahiba wake wa karibu mjini Unguja.

 

Banka amekuwa haonekani Yanga tangu asa­jiliwe msimu huu, huku baa­dhi wakihisi kwamba aliingia mitini kutokana na kutomal­iziwa mkwanja wake.

 

Lakini yeye mwenyewe licha ya kuitwa mara kadhaa kwenye mazoezi ya Yanga hajatokea, ame­kuwa akiwaambia waandi­shi kwamba anaumwa na anajitibia mwenyewe kwao. Jambo ambalo timu yetu ya waandishi ilifanya uchunguzi na kubaini kwamba jamaa kapigwa pini na Fifa kwa muda wa miezi mitatu.

Comments are closed.