The House of Favourite Newspapers

Mbao FC Yaweka Rekodi SportPesa

Wachezaji wa timu ya Mbao FC.

TIMU ya Mbao FC ya Mwanza imefanikiwa kuweka rekodi katika michuano ya SportPesa Cup kufuatia kuwatoa mabingwa watetezi wa michuano hiyo Gor Mahia kwa kuwafunga penalti 4-3 ambao walitwaa kombe hilo mara mbili mfululizo.

 

Gor Mahia ndiyo timu pekee ambayo imefanikiwa kutwaa ub­ingwa wa SportPesa tangu ilipoan­zishwa mwaka 2017 na kufanikiwa kucheza na timu ya Everton baada ya kupata ubingwa mara mbili.

 

Aidha, tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo, timu za Tanzania hazijawahi kutwaa ubingwa am­bapo mwaka jana Simba ilitinga fainali lakini ilitolewa na Gor Ma­hia, hivyo kuwapa nafasi wapin­zani wao hao kusonga mbele.

 

Hivyo, kutokana na matokeo ya juzi, Mbao ambao ndiyo mara yao ya kwanza kushiriki michuano hiyo, imefanikiwa kujiwekea rekodi ya kipekee kwa kuwa­toa mabingwa watetezi ambao walikuwa mwiba kwa timu za Simba na Yanga kwa miaka miwili mfululizo ambayo walishiriki na kuwapa nafasi ya kutwaa ubingwa huo.

 

Aidha, akizungumzia kutinga hatua ya nusu fainali, Kocha wa Mbao FC, Ally Bushiri ambapo watakutana na Karobangi Sharks, leo alisema:

 

“Niliandaa kikosi changu vizuri hasa katika suala zima la nidhamu ya mchezo na ndiyo maana tume­pata matokeo hayo, kwa sasa na­tambua nakutana na nani katika hatua ya nusu fainali nitakiandaa kikosi changu kuweza kushinda.”

Comments are closed.