The House of Favourite Newspapers

Suala La Beno, Yanga Lafika Patamu

Beno Kakolanya.

SUALA la kipa wa Yanga, Beno Kakolanya na klabu yake hiyo, limeingia katika sura mpya kufuatia kupelekwa katika Kamati ya Katiba Sheria na Hadhi za Wachezaji ili kupatiwa ufumbuzi.

 

Kakolanya aliingia katika mvutano na Yanga kufuatia kocha wa timu hiyo, Mwinyi Zahera kum­kataa katika kikosi chake kutokana na madai ya utovu wa nidhamu.

 

Kutokana na hilo, mlin­da mlango huyo aliomba mkataba wake uvunjwe jambo ambalo Yanga hawakulitekeleza, hivyo kuamua kuliwasilisha suala hilo kwa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) chini ya mwanasheria wake, Leonard Richard.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, Ofisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, alieleza kuwa: “Tumeipokea barua ya Beno hivi karibuni, tayari imewasilishwa katika Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ambayo itaku­tana kwa ajili ya kuli­jadili suala hilo na kufikia ufumbuzi.”

Stori: Khadija Mngwai, Dar es Salaam

Comments are closed.