Infinix Yasherehekea Na Wateja
Kampuni ya Simu za mkononi ya Infinix imefanya sherehe ya pamoja na wateja wake kufuatia mapokeo mazuri yao aina ya S5 ambayo ilizunduliwa hivi karibuni.
Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa sherehe hiyo iliyofanyika Ukumbi wa Tips uliopo Mikocheni Dar, Afisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Aisha Karupa amesema, wameamua kufanya pati hiyo na wateja wao ili kujadiana mambo mbalimbali kuhusiana na simu hiyo.
“Tumeamua kusherehea na wateja wetu kama njia moja ya kuwashukuru kwa kutuunga mkono katika ingizo letu hili jipya ambalo limepokelewa vizuri sana sokoni.
HABARI/PICHA: NEEMA ADRIAN/GPL