The House of Favourite Newspapers

Hadithi ya Eric Shigongo: Dimbwi la Damu-03

ERIC SHIGONGO: DIMBWI LA DAMU-03

GLOBAL PUBLISHERS

Nyumbani kwake sherehe iliendelea kama kawaida na Nicholaus aliendelea kuwamiminia rafiki zake juisi kama walivyoagizwa na mama yake, yeye hakunywa juisi kwa sababu alijua baba yake angemletea isicrimu kama alivyoagiza.

Martin ni kijana aliyefanikiwa sana katika maisha yake tena katika umri mdogo, anamuoa Hoyce msichana waliekutana nwaye katika ndege na Mungu anawajalia kupata watoto wawili mapacha, Nicholaus na Victoria! Ni familia yenye furaha ingawa Martin ni mtu wa kusafiri mara nyingi kwenye biashara zake.

Ilikuwa ni siku ya furaha akiwa nyumbani baada ya safari na kuwafanyia watoto wake skukuu ya kuzaliwa Wageni wamealikwa nyumbani kwa ajili ya sherehe hiyo, ni furaha tupu lakini fuaha hiyo inabadilika na kuwa kilio! Martin, Hoyce na mtoto wao Victoria wanapata ajali mbaya ya gari lao kugongwa na trewni la mizigo. Nyumbani hakuna mtu ambaye ana habari na tukio hilo sherehe bado inaendelea! Je, nini kitaendelea? Je, ajali hii ni ya kisasa? Endelea ……………

Nyumani sherehe iliendelea hadi saa mbili usiku bila Martin na mke wake pamoja na mtoto wao wa kike Vicky kurejea nyumbani, watu wengi waliokuwepo nyumbani walianza kuingiwa na wasiwasi mioyoni mwao, walishindwa kuelewa ni jambo gani lililotokea mpaka wakachelewa kiasi hicho! Pamoja na watu wote kuwa na wasiwasi bado Nicholaus aliendelea kucheza na watoto wenzake akijua wazazi wake wangerejea na kuendelea na sherehe kama kawaida.

“Kwanini baba na mama yako hawarudi?” Watoto wenzake waliuliza.

“Watarudi tu labda wamepita sehemu fulani!” Alijibu Nicholaus bila kujua kuwa baba, mama na Vicky walipata ajali mbaya ya kugongwa na treni.

“Njaa zinatuuma wangerudi tukala na kushiba kisha tuondoke!
Mpaka saa tatu na nusu za usiku walikuwa bado hawajarejea na wasiwasi ulizidi kuongezeka, hata Nicholaus na umri wake mdogo alianza kuhisi wazazi wake walikuwa wameptwa na tatizo fulani.

“Pigeni simu kwa baba mdogo namba ile pale labda watakuwa wamepita huko!” Alisema Nicholaus akionyesha namba ya simu iliyokuwa ukutani.

“kwani walikwenda wapi?” shangazi aliuliza

“Walikwenda kuchukua keki ya sikukuu ya Bathdei ya watoto wao!”
“Sikukuu yenyewe hamjatualika halafu mapiga simu kutuuliza, mnatujoki nini? Si wanajifanya matajiri wacha wamalize matatizo yao wenyewe wamezidisha sana maringo!” Alisema shangazi kwa ukali na kukata simu.
“Hawajaonekana!”Alisema mama huyo.

Baadaye saa nne usiku wageni waliokuwa kwenye tafrija hiyo walianza kuondoka kurejea majumbani kwao, uvumilivu ulianza kumshinda Nicholaus akaanza kulia, mtumishi wa ndani alianza kumbembeleza lakini hakunyamaza aliendelea kulia mpaka saa sita ya usiku.

“Usilie sana Nicky, watakuja tu!”
“Baba na mama wako wapi?”
“Watakuja tu!”
“Au wamepata ajali?”Nicholaus ajikuta akitamka maneno hayo bila kujua aliongea ukweli!
“Hapana hawezi kupata ajali,
baba huendesha gari vizuri!”

Relini:
Watu wengi walijaa eneo la ajali kushuhudia ajali ya treni kugonga gari, gari lilipondwapondwa na vipande vya miili ya watu vilisambaa kila mahali, ilikuwasi rahisi hata kidogo kuwatambua watu waliokuwa ndani ya gari hilo! Wasamaria wema walijaribu kulisoma gari hilo namba ili kujua ilikuwa gari la nani lakini hawakukiona kibao. Baadaye mtu mmoja aliokota kipande cha kioo alikisoma aliziona namba za gari hilo.

“Ni TZX 201745! Hili huwa la nani kweli?”
“Ni gari la Martin!”
“Yaani Martin ndiye amekufa?”
“Nina hakika ni yeye!”
Martin alikuwa ni maarufu mno mjini Arusha, kila mtu alimfahamu na hata gari lake aina ya Landcruiser lilifahamika na wengi, kila mtu aliyekuwepo eneo la ajali alisikitika kuona Martin alikufa kifo cha aina hiyo. Walipotazama vizuri kwenye gari waliona mkono wa mwanamke, kila mtu akajua alikufa pamoja na mkewe.

Wakati wakimsubiri trafiki wafike eneo hilo kupima ghafla kilisikika kilio cha mtoto, kutoka katika kichaka kilichokuwa jirani kabisa na eneo hilo!
Watu wote walishtuka, ilikuwa sauti ya mtoto akiomba msaada!
“Ba.. ba ni saa.. i..die.. nakufa!”

Watu wote walikimbia kwenda kwenye kichaka hicho cha miti ya michongoma, mtau mmoja aliingia hadi ndani bila woga na kilichofuata ni kelele za mtu huyo kutoka ndani ya kichaka.
“Jamani kuna mtoto humu ndani kaumia sana hebu njooni muone!”
“Mbebe utoke naye huku nje!”

Bila kupoteza muda mtu huyo alitoka na mtoto huyo hadi nje ya kichaka, uso wake ulijaa damu tupu na alikuwa na majeraha kila sehemu ya kichwa chake! Hakuwaona tena sababu ya kuendelea kuwasubiri trafiki, walimpakia mtoto huyo ndani ya gari la msamaria mwema na safari kwenda hospitali ya Mount Meru ilianza!

Mtoto huyo hakuongea kitu tena hadi walipofika hospitali ambako alipokelewa na kukimbizwa haraka chumba cha upasuaji ambako madaktari walifanya kila walichoweza kuokoa maisha yake, hakuna mtu hata mmoja aliyelifahamu jina la mtoto huyo na kwamba alikuwa mtoto wa nani!
Masaa matatu baada ya kuingizwa chumba cha upasuaji mtoto huyo alitolewa na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi ambako alilala bila kujitambua akivuta hewa kwa kutumia mashine ya oksijeni! Hakuna aliyekuwa na uhakika kuwa mtoto huyo angepona.

Pamoja na umri wake kuwa mdogo usiku wa siku hiyo Nicholaus hakupata hata lepe la usingizi, alilia mpaka sauti ikamkauka akiwalilia baba na mama yake pamoja na dada yake Vicky, hakubembelezeka hata kidogo! Masikio yake yalikua nje yakisikiliza kila kilichoendelea! Hata aliposikia paka au mbwa akipita alijua mama na baba yake pamoja na dada yake wanarudi, alinyanyuka na kukimbia hadi mlangoni lakini hakuna mtu aliyegonga mlango! Moyo wake ulizidi kuwa na wasiwasi zaidi alishindwa kuelewa wazazi wake walikuwa wapi na nini kiliwapata!

Leah, mfanyakazi wa ndani nyumbani kwao usiku mzima alimbeba mkononi mwake akizidi kumbembeleza lakini alizidi kulia kwa sababu Nicholaus alikuwa ni mtoto aliyependa sana kuangalia televeheni hasa vipindi vya wanyama, Leah alimamua kumuwashia luninga ili aangalie wanyama lakini badala ya kukuta kipindi cha wanyama alikuta ni taarifa ya habari na kuamua kuingalia ingawa hakupanga!

“Ajali mbaya ya treni!” Ndivyo alivyoanza msoma taarifa ya habari wa siku hiyo na baadaye kuendelea “Jana majira saa moja jioni gari aina ya Landecruiser lenye namba za usajili TZX 201745 Liligonga treni la mzigo lililokuwa safarini kutoka maeneo ya viwandani kurejea kituo cha reli cha Arusha, miili ya watu wawili ikiwa iimepondekapondeka imeokotwa eneo la ajali gari likiwa limeharibika vibaya na si rahisi kulitambua! Mtoto mdogo mwenye umri wa miaka kati ya mitano na sita ambaye inaaminika alikuwemo katika gari lililogongwa aliokotwa katika kichaka akiwa amejeruhiwa vibaya na sasa amelazwa katika hospitali ya Mount Meru, hali yake ikiwa mbaya.

Mpaka tunatangaza taarifa hii watu waliokufa na hata mtoto huyo bado hawajatambulika kwa majina! Uongozi wa hospitali ya Mount Meru unawaomba waliopotelewa na ndugu zao wafike hospitali ya Mount Meru kutambua miili ya marehemu na pia mtoto huyo ambaye hivi sasa amelezwa katika wodi ya wagonjwa mahututi!!!” alimaliza msomaji huyo.

Picha ya gari la Martin ilionekana likiwa limegongwa na kuharibiwa vibaya! Leah hatutaka Nicholaus aione picha hiyo, alimfunika usoni kwa kiganja ili asione lakini tayari Nicholaus alishaona na kuanza kulia.
“Dada! Baba na mama gongwa na treni?
“Hapana!”
“Si nimesikia na gari la baba nimeliona?”

Leah alikosa cha kumjibu, alichofanya ni kumbeba Nicholaus mgongoni na kutoka nje ya nyumba akafunga mlango na kumwomba mlinzi amsindikize kwenda hospitali ya Mount Meru, kabla hajatoka mlangoni alikutana na majirani wengi pamoja na marafiki wa Martin wakija nyumbani kwao baada ya kuiona taarifa ya habari katika luninga!
“Leah!”
“Naaam!”
“Umesikia taarifa ya habari?”
“Ndiyo!”
“Hivi kweli lile gari ni la baba yako?”
“Ni kweli kwani tangu waondoke jana kwenda kutafuta keki ya Bethidei ya watoto wao hawajarudi!”
“Hawakurudi?” Aliuliza mmoja wa majirani aliyekuwepo jana yake wakati wa tafrija!
“Ndiyo!”
“Basi ni lazima twende huko hospitali upesi kuhakikisha!”

Wote walitoka na kuingia ndani ya gari na safari ilianza haraka sana kuelekea hospitali ya Mount Meru, muda wote wa safari Nichoulaus aliwalilia wazazi wake.

Walipofika hospitali waliuliza mapokezi na kuelekezwa mahali alikolazwa mtoto aliyetangazwa redioni na kwenye television!

“Alipoletwa hapa hali yake ilikuwa mbaya sana haikuwa rahisi hata kulitambua jina lake, ila amelazwa chumba cha wagonjwa mahututi baada ya upasuaji twendeni niwapeleke alipo!” alisema muuguzi mmoja na kuondoka nao.

Walitembea na walipofikia jengo la wodi ya wagonjwa mahututi waliingia moja mwa moja hadi ndani na kuonyeshwa mtoto alipolala!
“Maskini Vicky!” Leah alishindwa kuvumilia baada ya kumuona Vicky katika hali aliyokuwa nayo alimwaga machozi na kutaka kuanguka juu ya kitanda na kumkumbatia lakini muuguzi alimshika kabla hajafanya hivyo, kilio cha Nicholaus aliyekuwa mgongoni mwa dada yake kilikuwa si rahisi kukielezea, alilia huku akiliita jina la dada yake na bado alitaka aonyeshwe mahali walipokuwa baba na mama yake.

“Wako wapi baba na mama wangu!” aliuliza Nicholaus huku akitokwa na machozi, alimtia huruma kila mtu aliyemwona, alionyesha wazi pamoja na umri wake kuwa mdogo ni kiasi gani aliumia moyoni mwake.

Kumwona Vicky kuliwafanya waamini na kuwa na uhakika kuwa hata waliokufa walikuwa ni Martin na Hoyce!! Kila mtu alilia machozi ya uchungu ilikuwa si rahisi kuamini kuwa mwisho
wa maisha yao ungekuwa ule! Walikuwa tayari kuamini baada ya kuiona miili yao!
Kutoka wodini huku wengi wao wakilia waliongozana moja kwa moja kuelekea chumba cha maiti ambako waliomba waonyeshwe miili ya ndugu zao, ilikuwa kazi ngumu sana kukubali
kuwa maiti walizoonyeshwa zilikuwa ni za Martini na Hoyce, kwani ziliharibiwa vibaya mno zilikuwa ni vipande vilivyokusanywa pamoja! Walilazimika kuamini hivyo sababu walikwashamuona Vicky wodini!

Majirani waliondoka chumba cha maiti kurudi nyumbani wakilia na kwenda nyumbani ambako walitangaza msiba! Leah na Nicholaus walibaki wodini pembeni mwa kitanda cha Vicky.

Mamia ya watu walikusanyika nyumbani kwa Martini kuomboleza kifo cha kijana aliyekuwa na umaarufu mkubwa mjini Arusha baada ya kupata utajiri katika umri mdogo! Lilikuwa ni jambo la kusikitisha sana na karibu kila mtu aliyekuwepo nyumbani pale alilia machozi ya uchugu

Wazazi wa marehemu Martini waliofariki miaka mitano kabla ya kifo chake na katika tumbo la mama yake walizaliwa watoto watatu yaani Mrtini , dada yake Christina na mdogo wake wa kiume Alphonce! Baada ya kufariki wazazi wao walioishi kijijini Bupandwamhela wilayani Sengerema mkoani Mwanza. Martini aliyeishi Arusha aliamua kuwahamisha ndugu zake kuwapeleka Arusha ambako aliwapa mitaji ya kufanyia biashara.

Walihama pamoja na familia zao, Christina aliyezaa watoto watatu kabla ya kuolewa alihama na watoto wake na Alphonce aliyekuwa na wake wawili na watoto wanne alihama nao kwenda Arusha, kwa wema wake Martin aliwanunulia kila mtu nyumba yake wakaishi maisha ya raha mustarehe.

Baada ya kufika Arusha Alphonce alianza biashara ya madini ya Tanzanite aliyofanya kaka yake lakini kwa sababu ya kuzidisha starehe na ulevi baada ya muda mfupi mtaji wake ulikwisha, akarudi tena kwa nduguye na kupewa shilingi milioni tatu lakini nazo pia alizimaliza katika ulevi na wanawake!

Christina naye baada ya kupewa Milioni tano na kaka yake alimpenda kijana mdogo wa Kimasai na kumkabidhi pesa zote kijana huyo alizitumia katika starehe zake mpaka zikaisha, alirudi tena kwa kaka yake na kupewa milioni mbili zaidi nazo zilipondwa na mpenzi wake.

Mara tano mfululizo Martin alitoa pesa kuwasaidia ndugu zake lakini alikata tamaa na kuamua kuwaacha kama walivyo, muda mfupi baadaye alimuoa Hoyce ndiyo chuki ikaongezeka kati yake na nduguze wakidai alichotwa akili na mwanamke wa Kichaga na kuwasahau ndugu zake.
Kwa huruma zake Martin ndugu zake walipopata shida nyingi aliamua kuwapa kazi katika machimbo yake huko Mererani na kuwalipa mishahara kama wafanyakazi wengine ili waendeshe maisha yao sababu hawakuwa na sehemu yoyote ya kwenda! Hiyo nayo haikutosha walifanya ukorofi kazini ikabidi awasimamishe kazi.

Je, nini kitaendelea?
Kwa sababu Jumanne haikutoka na kutoka leo! Kesho nitaweka muendelezo wake kama kawaida.
Usisahau kuSHARE kwa ajili ya marafiki zako.

Comments are closed.