Hatimaye mwili wa aliyekuwa msanii wa Bongo Movie, Gift John aliyefariki juzi katika Hospitali ya Sinza- Palestina baada ya kuugua, umezikwa leo katika Makaburi ya Kinondoni.
Kabla ya mazishi, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie walipata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa marehemu, shughuli iliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Njiapanda ya Segerea, Dar ambapo wasanii wengi wa tasnia ya filamu Bongo walihudhuria.
Marehemu Gift, pia alikuwa ni mke wa muongozaji maarufu wa filamu, John Lister. baada ya ibada fupi iliyofanyika nyumbani marehemu, mwili wa Gift ulipelekwa Makaburi ya Kinondoni ulikopumzishwa.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina!
Na Denis Mtima/ GPL
Comments are closed.