The House of Favourite Newspapers

Watano Wafa Ajali ya Lori na Noah Dodoma

0

WATU watano  wamefariki na wawili  kujeruhiwa baada ya gari dogo aina ya Noah lililokuwa likitokea Morogoro kwenda Dodoma kugongana na lori eneo la Kibaigwa jijini Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa  Dodoma, Gilles Muroto amethibitisha tukio hiloo na kusema imesababishwa na uzembe wa dereva wa lori ambaye aliingia katikati ya barabara akitokea kwenye kituo cha mafuta bila kuangalia pande zote za barabara na kusababisha Noah kuingia uvunguni mwa lori.

Pia ameeleza kuwa dereva wa lori ametoroka na jeshi la polisi linaendelea kumsaka huku likifanya uchunguzi zaidi wa ajali hiyo.

Kuhusu majeruhi wawili wa ajali hiyo, Muroto amesema mmoja ana hali mbaya zaidi na juhudi za madaktari zinaendelea katika kunusuru uhai wake.

Leave A Reply