The House of Favourite Newspapers

Amani lafika Tandale, wasomaji wachangamkia ‘Shinda Nyumba’

0

1.Athumani Hemed (kushoto) mkazi wa Tandale sokoni  akijaza kuponi  kushiriki bahati nasibu ya Shinda Nyumba. Anayemshuhudia ni Ofisa Masoko wa Global, Yohana Mkanda.

2Selemani Amir (kulia) akipewa maelekezo na Mkanda namna ya kujaza kuponi yake.

3.Juma Kambi (wa pili kulia) akijaza kuponi yake.

4.Omary Hatibu akijaza kuponi kushiriki droo kubwa ya bahati nasibu ya Shinda Nyumba.

5.Mhina Salum (kulia) akijaziwa kuponi na Ofisa Masoko wa Global, Yohana Mkanda.

6Mkanda akizidi kuwasaidia kujaza kuponi zao wasomaji wa gazeti la Amani ili kushiriki bahati nasibu hiyo.

7.Yahya Ramadhan akisaidiwa kujaza kuponi na Mkanda.

8…Akimtajia namba yake ya simu Mkanda ili iandikwe katika kuponi hiyo.

9.Fred Peter (kulia) akishiriki kujaza kuponi ya bahati nasibu.

10.Hussein Kadudu (kushoto) akijaza kuponi, anayemshuhudia ni Yohana Mkanda.

11.Mkanda akimjazia kuponi mdau wa gazeti la Amani aliyejitambulisha kwa jina la Abbas Fundi.

12. Mkanda akimwelekeza msomaji wa Gazeti la Amani namna ya kuajaza kuponi ili kushiriki bahati nasibu ya Shinda Nyumba.…Akimwelekeza msomaji wa gazeti la Amani, Ally Mohammed, namna ya kujaza kuponi ili kushiriki bahati nasibu ya Shinda Nyumba.

BAHATI nasibu ya ‘Shinda Nyumba’ ikiwa imebakiza siku chache tu kuchezeshwa leo Alhamisi  promosheni  ya shindano hilo iliwafikia  wakazi wa Tandale na maeneo mengine jijini Dar  waliojitokeza  kwenye gari la matangazo walipochangamkia kununua Gazeti la Amani na kushiriki kujaza kuponi za bahati nasibu.

Bahati nasibu hiyo inaendeshwa na Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Championi, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda.

Akizungumza na wakazi eneo hilo, Ofisa Masoko wa Global Publishers,Yohana Mkanda alisema kuwa zimebaki siku sita hivyo wachangamkie fursa hiyo kwani inaweza kuwa nyumba hiyo mionmghoni mwa wana Tandale.

Katika uhamasishaji huo, Yohana Mkanda alirudia wito wake kwamba: “Siku zimebaki sita nunueni magazeti ya Global mengi na mjaze kuponi ili kujiongezea nafasi ya kushinda nyumba kwani unaweza kuwa wewe au yule na kugeuka baba au mama mwenye nyumba! Hivyo, fursa ndiyo hii, bahati humjia mtu yeyote, kwa hiyo nunua magazeti yetu pendwa yaliyojaa bahati na kila namna kila wakati. Kazi kwako, nyumba ndiyo hiyoo…!!!”

NA DENIS MTIMA/GPL

Leave A Reply