Gazeti la Amani ambalo linachapishwa na Global Publishers pamoja na magazeti ya Championi, Uwazi, Risasi, Ijumaa, pamoja na Ijumaa Wikenda leo limegawa zawadi ya kiasi cha pesa shilingi 10,000 kwa wauza magazeti ambao wamekuwa wakifanya vizuri kimauzo.
Amani lilitembelea mitaa ya Morocco jijii Dar na kumpa zawadi Richard Daud, ambapo mitaa ya Kinondoni zawadi ilikwenda kwa Msafiri Geofrey na mitaa ya Temeke- Mwembe Yanga lilimpa zawadi Mohammed Machela.
Stori: Boniphace Ngumije