The House of Favourite Newspapers

Amber Lulu Aanika Alivyoshea Bwana na Gigy!

DAR ES SALAAM: Msanii wa Bongo Fleva, Lulu Eugen ‘Amber Lulu’ amefunguka suala la kushea bwana na msanii mwenzake, Gift Stanford ‘Gigy Money’.

Amber Lulu amesema kuwa, ni kweli aliwahi kushea mwanaume mmoja na Gigy Money siku za nyuma.

 

“Kutokana na lifestyle yangu ya sasa hivi, watu hawamjui bwana’ngu kwa hiyo wanajitahidi kumtafuta na kuotea kama natoka na nani.

“Mimi sijawahi kugombana na mtu, hizo stori za kugombea mwanaume ni zamani sana, kama miaka mitatu au miwili huko nyuma.

 

“Nakumbuka mwanaume ambaye mimi nilipita naye na yeye (Gigy) akapita naye ni Casto Dickson,” alisema Amber Lulu.

 

Msanii huyo amezungumzia suala la wanawake kudanga ili wapate pesa ambapo amesema kuwa.

“Inatokeaga mara nyingi sana, Bongo hakuna mwanamke awe na mtu halafu akatae pesa, kila mtu anategemea mwanaume mwenye pesa, halafu sisi wanawake tunapenda kupewa ila inategemea unadanga kiasi gani,” alisema Amber Lulu.

Stori: Neema Adrian, Ijumaa

Comments are closed.