The House of Favourite Newspapers

Amber Rose Atambulishwa Ukweni

1
21 Savage, (24) akiwa na mpenzi wake Amber Rose wakionesha wapo siriazi katika uhusiano wao wa kimapenzi.

 

RAPA anayetikisa na Albamu ya Issa, 21 Savage, (24) ameonesha kuwa siriazi katika uhusiano wake wa kimapenzi na Mwanamitindo Amber Rose, (33) baada ya kumpeleka kumtambulisha ukweni.

 

Tukio hilo ‘amaizing’ lilijiri juzikati ambapo 21 Savage aliamua kuvunja ukimya kwa kumpeleka nyumbani kwao na kumtambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.

 

Baada ya kutambulishwa, Amber alionesha kuwa na furaha na kutupia picha nyingi mitandaoni wakipata chakula pamoja na nyingine wakiwa katika pozi na mama wa 21 Savage.

 

Hivi karibuni, 21 Savage alihojiwa juu ya kuwa na uhusiano na Amber na kufunguka; “Ni msichana mtulivu…ananifanya nijione kama King na hajawahi kugombana na mimi.” 2013, Amber aliolewa na rapa Wiz Khalifa na kufanikiwa kupata mtoto mmoja, Sebastian lakini walikuja kuachana 2016.

1 Comment
  1. […] ukweni ghafla unaona wanakimbiza kuku bila kujua chochote unaropoka, “Jamani eeehh… huyo apikwe na […]

Leave A Reply