Amberr Washington Aifagilia Global Group (Picha +Video)
MAKAMU wa Rais wa Tuzo za Hollywood and African Prestigious (HAPA) kutoka Marekani, Amberr Washington, ametua ndani ya mjengo wa Global Group, Sinza-Mori jijini Dar na kueleza namna walivyojipanga kutoa fursa kwa vijana wenye vipaji mbalimbali nchini Tanzania.
Amber amewapongeza wafanyakazi wa Global Group kwa namna walivyompokea na jinsi wanavyofanya kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu.
Mmarekani huyo mwenye asili ya Afrika, alikuwa ameongozana na Balozi wa Tuzo hizo nchini ambaye pia ni mmiliki wa Master Tanzania, Mawini Casy, na mbunifu wa mavazi nchini, Martin Kadinda, Ofisa Sanaa wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Henry Mrutu na ofisa Sanaa Mwandamizi wa Basata, Godffrey Nago.
Comments are closed.