The House of Favourite Newspapers

Amuua Mwenzake Wakigombea Kumbikumbi

MURIUNGI KIYOGERE (35), mkazi wa Kaunti ya Tharaka-Nithi nchini Kenya, anadaiwa kumchoma kisu mara nne Daniel Mutiria Cece (36) kutokana na mzozo wa kugombea kumbikumbi Jumapili jioni.

Kamanda wa Polisi wa Tharaka Kusini, Kiprop Rutto,  alisema mshukiwa alikimbilia katika Kituo cha Polisi cha Marimanti kuwakwepa wanakijiji waliokuwa wakitaka kumuua.

Mshukiwa alizuiliwa kituoni hapo baada ya kukiri kuua na  polisi walipokwenda eneo la tukio walikuta mwili wa Daniel ukiwa umelowa damu.

Inadaiwa wanaume hao walikuwa marafiki wa miaka mingi na kabla ya ugomvi kutokea walikuwa pamoja wakinywa pombe.

Comments are closed.