The House of Favourite Newspapers

Apple Kutoa Punguzo Ununuzi wa Betri Mpya za Simu

MTENDAJI mkuu wa kampuni ya Apple, Tim Cook, amewaomba radhi wateja wake kuhusiana na kwamba simu za kampuni hiyo hupungua nguvu za utendaji wake kutokana na betri zinazoisha muda wake haraka.

 

Cook ameahidi kwamba, siku zijazo, Apple “itatoa kipaumbele zaidi kuhusiana na nguvu ya betri za simu aina ya iPhone” na kuwaacha watumiaji wake waone iwapo muda mrefu wa betri hizo utaathiri utendaji wa simu zao. Apple inatoa punguzo katika manunuzi ya betri mpya kwa yeyote mwenye iPhone 6 au nyingine, ilisema kampuni katika taarifa yake.

 

Betri mpya itagharimu Dola 29 (Tsh. 58,000) badala ya Dola 79 (Tshs 176,000) kuanzia Januari mwaka 2018. Punguzo hilo linatia maanani pia mahitaji ya maduka ya watengenezaji wa simu. Wakati ujumbe huo wa Cook ulikuwa unawataka radhi wateja, bado alikana kwamba Apple hupunguza kasi ya utendaji wa simu hizo ili kuwalaziisha watu kununua simu mpya.

 

“Kitu cha kwanza na muhimu zaidi ni kwamba kamwe hatujafanya na hatutafanya chochote cha kupunguza makusudi muda wa utendaji kazi wa bidhaa za Apple, au kumlazimisha mteja anunue bidhaa nyingine,” alisema. Kampuni hiyo huko nyuma iliwahi kusema kwamba iwapo isingepunguza utendaji kazi wa simu hizo, betri za zamani zilikuwa zinakabiliwa na tishio la kuzima ghafla.

 

Kwa mujibu wa wataalam, maelezo hayo yalikuwa ya kiufundi. Tamko hilo la Apple la wiki iliyopita kwamba hupunguza utendaji kazi wa simu hizo, liliibua shutuma nyingi na watu kufungua kesi. Kampuni moja ya Ufaransa inayopigania haki za wateja, ilifungua kesi wiki hii (Desemba 27) kuishitaki Apple kwa kupunguza nguzu za simu zake za zamani ili kupata fursa ya kuuza mpya.

 

Nchini Ufaransa, ni haramu kupunguza ubora wa bidhaa za zamani ili kupromoti mauzo ya bidhaa mpya. Kesi hiyo iliyofunguliwa na kundi la Halte à l’Obsolescence Programmee, ina uwezekano wa mshitakiwa kutumikia kifungo cha miaka miwili gerezani.

Comments are closed.