STORI: GABRIEL NG’OSHA | RISASI | MIKITO NUSUNUSU
IKIWA ni miaka nane sasa tangu mama mzazi wa Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Ambwene Yessayah ‘AY’, Lydia Bizima afariki dunia, staa huyo ameibuka na kueleza urithi alioachiwa na mama yake. Akibonga na Mikito Nusunusu , AY alisema enzi za uhai wa mama yake alikuwa akimuhusia sana kuhusu kujiamini, kujituma ambapo kila
anapoyakumbuka maneno hayo, anajikuta akipata nguvu na kufanya mambo makubwa na mazuri zaidi. “Mama yangu kipenzi aliniachia urithi mzuri kwani mara nyingi alikuwa akinisisitizia kuwa ni lazima nijiamini, nijitume na nifanye kazi nzuri kwa sababu yeye pia alikuwa anajiamini sana na mpiganaji hivyo nimeufanyia kazi ndiyo maana niko hivi nilivyo leo,” alisema AY
Shinda Nyumba Awamu ya Pili Yatikisa Jiji la Dar es Salaam
Comments are closed.