Azam waichapa Esperance 2-1
Patashika wakati wa mtanange wa Azam dhidi ya Esperance leo.
Ramadhan Singano ‘Messi’ akimiliki mpira pembeni ya wachezaji wa Esperance.
Mmoja wa wachezaji wa Esperance akipatiwa huduma ya kwanza uwanjani.
Mashabiki wa Esperance wakiishangilia timu yao.
Kipre Tchetche akimtoka beki wa Esperance.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye (kulia) na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Lameck Nchemba nao walikuwepo kushuhudia mpambano huo.
TIMU ya Azam FC leo imeibuka kidedea kwa kuifunga Esperance ya Tunisia mabao 2-1 kwenye mchezo wa raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho Afrika uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar.
Mabao ya Azam yamewekwa kimiani na Farid Mussa katika dakika ya 68 na Ramadhan Singano ‘Messi’ aliyefunga bao la pili dakika ya 69 ya mchezo.
Bao la Esperance limefungwa na Haithem Jouini dakika ya 33.
(Picha zote na Sweetbert Lukonge / GPL)
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, INGIA NA LIKE PAGE YA FACEBOOK YA ERIC SHIGONGO===>https://www.facebook.com/shigongotz/
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA TUFOLLOW
INSTAGRAM===>https://www.instagram.com/globalpublishers/
TWITTER===>https://twitter.com/GlobalHabari
FACEBOOK===>https://www.facebook.com/GlobalPublishers
YOU TUBE===>https://www.youtube.com/user/uwazi1