The House of Favourite Newspapers

Baada ya Kuzushiwa Kulala Makaburini, RC Hapi Atoa Tamko

MKUU wa Mkoa wa Iringa, Ally Salum Hapi amekanusha taarifa za uzushi zilizotungwa dhidi yake na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa mwezi uliopita alikuwa amelala ndani nyumbani kwake usiku lakini kulipokucha alijikuta amelala makaburini na kukimbilia Dar es Salaam na mpaka sasa hajarudi tena Iringa.

 

Hapi amemtaka mtu aliyetunga na kusambaza uzushi huo akajisalimishe yeye mwenyewe kwa Mkuu wa P0lisi  wa Mkoa (RPC) wa Iringa, Juma Bwire,  kabla ya Desemba 21, mwaka huu saa 2:00 asubuhi.

Comments are closed.