The House of Favourite Newspapers

Banana atingisha uzinduzi wa Jozi Lounge

0

1 Mkurugenzi Mtendaji wa klabu ya Jozi Lounge,  Dismas  Massawe, akikata utepe kuashiria shughuli ya uzinduzi wa klabu hiyo.
2Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Banana Zorro, akitoa burudani muda mfupi baada ya uzinduzi wa klabu hiyo.
3Baadhi ya mashabiki waliohudhuria uzinduzi huo wakiingia ndani ya klabu hiyo baada ya kuzinduliwa.

4Mbunifu wa mavazi nchini,  Rhemtulah (kulia) akiwa na jamaa zake kwenye uzinduzi huo.

5Baadhi ya waalikwa  kwenye uzinduzi huo wakiwa katika pozi.6Mtangazaji maarufu Tayana (kulia), akiwa katika pozi na wenzake.
7Mashabiki wakiwa ndani ya Jozi Lounge.

8Wadau wa klabu hiyo wakiwa katika pozi.9Tayana akiwa kwenye pozi.10Wadau wa Jozi Lounge wakiwa kwenye zulia jekundu (red carpet).
11Dismas Massawe (kulia), akipozi mbele ya kamera.12Wageni Red Carpet.
13Baadhi ya warembo waliohudhuria uzinduzi huo wakiwa kwenye pozi.14Mapozi yalitawala kwa mashabiki waliofika hapo.

15Wadau wa ‘mastarehe’ wakiwa kwenye pozi.16Waalikwa wakiingia ndani ya Jozi Lounge muda mfupi baada ya uzinduzi huo kufanyika.

STAA wa muziki wa Bongo Fleva anayeupiga kwa njia ya bendi, Banana Zahir Zorro, usiku wa kuamkia jana aliwapagawisha vilivyo  mashabiki wake kwenye uzinduzi wa klabu mpya ya burudani ya Jozi Lounge iliyopo Msasani Village karibu na shule ya msingi Msasani jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo uliokatwa utepe na mmiliki wa klabu hiyo, Dismas Massawe, ulifanyika usiku mnene huku ukishuhudiwa na mamia ya mashabiki wa burudani ambao walijitokeza ambapo Banana  kupitia timu yake ya B-Band alisongesha burudani.

Akifanya makamuzi  muda mfupi tu baada ya  uzinduzi kufanywa, Banana  alitangaza kuwa kila siku ya Jumamosi bendi yake itakuwa ikifanya makamuzi hapo, hivyo akawataka mashabiki wajitokeze kwa wingi ili  kupata burudani ya kipekee.

“Nimefurahi sana leo kukutana na mashabiki wangu kwenye tukio hili la uzinduzi hivyo nitumie fursa hii pia kuwatangazia kwamba tutakuwa tukitumbuiza hapa kila siku ya Jumamosi, hivyo naomba mashabiki wangu wote tuwe tunakutana hapa kupata muziki mzuri na vinywaji safi kwa bei poa,” alisema Banana Zorro.

Habari/Picha: Musa Mateja/GPL.

 

 

Leave A Reply