Banana atingisha uzinduzi wa Jozi Lounge
Mkurugenzi Mtendaji wa klabu ya Jozi Lounge, Dismas Massawe, akikata utepe kuashiria shughuli ya uzinduzi wa klabu hiyo.
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Banana Zorro, akitoa burudani muda mfupi baada ya uzinduzi wa klabu hiyo.
Baadhi ya mashabiki waliohudhuria uzinduzi huo wakiingia ndani ya klabu hiyo baada ya kuzinduliwa.
Mbunifu wa mavazi nchini, Rhemtulah (kulia) akiwa na jamaa zake kwenye uzinduzi huo.
Baadhi ya waalikwa kwenye uzinduzi huo wakiwa katika pozi.Mtangazaji maarufu Tayana (kulia), akiwa katika pozi na wenzake.
Mashabiki wakiwa ndani ya Jozi Lounge.
Wadau wa klabu hiyo wakiwa katika pozi.Tayana akiwa kwenye pozi.Wadau wa Jozi Lounge wakiwa kwenye zulia jekundu (red carpet).
Dismas Massawe (kulia), akipozi mbele ya kamera.Wageni Red Carpet.
Baadhi ya warembo waliohudhuria uzinduzi huo wakiwa kwenye pozi.Mapozi yalitawala kwa mashabiki waliofika hapo.
Wadau wa ‘mastarehe’ wakiwa kwenye pozi.Waalikwa wakiingia ndani ya Jozi Lounge muda mfupi baada ya uzinduzi huo kufanyika.
STAA wa muziki wa Bongo Fleva anayeupiga kwa njia ya bendi, Banana Zahir Zorro, usiku wa kuamkia jana aliwapagawisha vilivyo mashabiki wake kwenye uzinduzi wa klabu mpya ya burudani ya Jozi Lounge iliyopo Msasani Village karibu na shule ya msingi Msasani jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi huo uliokatwa utepe na mmiliki wa klabu hiyo, Dismas Massawe, ulifanyika usiku mnene huku ukishuhudiwa na mamia ya mashabiki wa burudani ambao walijitokeza ambapo Banana kupitia timu yake ya B-Band alisongesha burudani.
Akifanya makamuzi muda mfupi tu baada ya uzinduzi kufanywa, Banana alitangaza kuwa kila siku ya Jumamosi bendi yake itakuwa ikifanya makamuzi hapo, hivyo akawataka mashabiki wajitokeze kwa wingi ili kupata burudani ya kipekee.
“Nimefurahi sana leo kukutana na mashabiki wangu kwenye tukio hili la uzinduzi hivyo nitumie fursa hii pia kuwatangazia kwamba tutakuwa tukitumbuiza hapa kila siku ya Jumamosi, hivyo naomba mashabiki wangu wote tuwe tunakutana hapa kupata muziki mzuri na vinywaji safi kwa bei poa,” alisema Banana Zorro.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL.