Barca ‘Yaitumbua’ Arsenal UEFA
Messi (katikati) akijaribu kuwatoka mabeki wa Arsenal Gabriel (kushoto) na Mohamed Elneny.
KIKOSI cha Arsenal usiku wa kuamkia leo kimeaga michuano ya Klabu Bingwa Ulaya ‘UEFA’ baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Barcelona kwenye mechi ya marudiano iliyopigwa Nou Camp, Barcelona.
Mabao ya Barcelona yaliwekwa kimiani na Neymar dk 18, Luis Suarez dk 65 na Lionel Messi dk 88 huku la Arsenallikifungwa na Mohamed Elneny dk 51.
Kwa matokeo hayo ya 3-1, Arsenal wamefungasha virago kwa kipigo cha jumla ya mabao 5-1.
Neymar akimalizia pasi ya Luis Suarez na kuifungia timu yake balo la kwanza.Sanchez (wapili kulia) akishindwa kuitumia nafasi vizuri na kukoswa bao la wazi.
Wenger akionesha kutofurahia matokeo aliyoyapata. Kikosi cha Barcelona wakishangilia. Elneny akijitutumua kulenga langoni. Shuti la Elneny likitolewa nje na golikipa wa Barcelona.
goalkeeper Kipa wa Arsenal, Ospina akishangaa mpira uliopigwa na Suarez ukizama langoniKikosi cha Barca kilichoitumbua Arsenal jana.
Mnyama, Luis Suarez akijikunja kuipatia timu yake bao la pili. Suarez baada ya kufunga bao la pili, akishangilia na Jordi Alba (kulia).
Bao la tatu, Lionel Messi akiachia shuti lililomshinda kipa wa Arsenal, David Ospina na kuingia langoni.
Bao la Suarez lilivyotokea. Meneja wa Barcelona, Luis Enrique akicheki mechi bila wasiwasiMjeruman, Ozil akiondoka na mpira.
Sanchez na Ozil wakisubiri kuanzisha mpira baada ya bao la kwanza la Neymar. Alex Iwobi wa Arsenal forward (kulia) akijaribu kupiga shuti golini.