The House of Favourite Newspapers

Barcelona Kumkosa Staa Huyu kwa Msimu Mzima Baada ya Majeruhi

Mchezaji wa klabu ya Barcelona Alex Vidal atakua nje ya uwanja kwa muda wa miezi mitano baada ya kupata majeraha eneo la kifundo cha mguu hapo siku ya jumamosi Februali 12, alipokua akiitumikia klabu yake katika mchezo wa ligi kuu nchini hispania dhidi ya Alaves katika dimba la Estadio de mendizorroza.

Vidal ambaye ana umri wa miaka 27, hucheza nafasi ya beki wa kulia aliumia mnamo dakika ya 85 ya mchezo wakati akiwania mpira na mchezaji wa Alaves Theo Hernandez.

Klabu ya Barcelona imethibitisha kumkosa beki huyo kwa msimu mzima baada ya kupata taarifa kutoka kwa madaktari wa timu hiyo hapo jana.

Comments are closed.