The House of Favourite Newspapers

Basata Yatengua Maamuzi ya Sakata la Miss Tanzania Kwenda Miss World

0

Baraza la Sanaa la Taifa – BASATA limesema halijaridhia na halijakubaliana na maamuzi ya kumuengua Miss Tanzania 2020/21 Rose Manfere kwenye ushiriki wa shindano la Dunia (Miss World 2021) mpaka pale Kamati ya Miss Tanzania itakapotoa sababu za msingi na kuzithibitisha.

 

Aidha BASATA limeilekeza kampuni ya “The Look” ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania kuwasilisha jina la Miss Tanzania 2020/21 (Rose Manfere) katika shindano la Urembo la Dunia (Miss World 2021) Hii imekuja kufuatia Kamati ya mashindano ya Miss Tanzania kutangaza kumuengua Miss Tanzania 2020/21 kwenye mashindano ya Urembo ya dunia na nafasi yake kuchukuliwa na mshindi wa pili, Juliana Lugumisa.

 

Leave A Reply