The House of Favourite Newspapers

Basi la Harusi Laua Watu 10 na Kujeruhi Wengine 25, Polisi Wamfungulia Mashtaka Dereva

0

WATU 10 wamefariki dunia na wengine 25 wamelazwa hospitalini baada ya basi la harusi kuanguka katika eneo la mvinyo nchini Australia.

Abiria hao walikuwa wakirejea kutoka kwenye harusi katika eneo la mvinyo Jumapili usiku katika eneo la Hunter Valley, eneo maarufu kwa watalii wa mvinyo, wakati kocha wao alipopinduka.

Polisi wamemfungulia mashtaka dereva huyo wa basi mwenye umri wa miaka 58 kwa makosa 10 ya kuendesha gari hatari na kusababisha kifo.Walisema kuwa bado wako katika harakati za kuwatambua waliofariki.Hata hivyo, watu hao wapya hawakuripotiwa kuwa kwenye basi hilo.

Kamishna wa polisi Karen Webb amesema eneo la ajali hiyo bado ni eneo la uhalifu. Maafisa wa upelelezi wanaoshughulikia eneohilo la ajali wakiwemo pia maafisa wa uokoaji

Kwa mujibu wa polisi, ajali hiyo ilitokea wakati, kukikuwa na ukungu mzito katika eneo hilo. Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese amesema ni ajali hiyo ni katili sana, wa kusikitisha na usio wa haki” kwa “siku ya furaha katika sehemu nzuri kama hiyo ili kuishia na kupoteza maisha ya kutisha”.

Leave A Reply