David Beckham na mwanaye Cruz Beckham
MWANASOKA wa zamani wa Man United ya England na Madrid ya Hispania, David Beckham na mkewe Victoria inasemekana wanamuandaa kijana wao mdogo Cruz mwenye umri wa miaka 11 kuwa Justine Bieber mpya kwenye anga la muziki duniani.
Tetesi hizo zimeibuka kufuatia kusambaa video mbalimbali zinazomuonesha Cruz akiimba nyimbo za wasanii wakubwa duniani zikiwemo When I’m Gone na Pitch Perfect wa Anna Kendrick huku akionesha uwezo mkubwa kama ilivyokuwa kwa Justine Bieber akiwa na umri kama huo.