Bendi ya SMG yatimiza miaka 4 ya uimbaji
Mmoja wa waimbaji wa bendi hiyo akifanya yake.
Picha matukio ya sherehe ya kutimiza miaka minne ya bendi ya SGM. BENDI ya Soul.
Gospel International ‘SMG’ ya Kawe jijini Dar, jana Jumapili ilisherehekea kutimiza miaka minne katika huduma ya uimbaji.
Sherehe hiyo ilifanyika katika Kanisa la Living Watels lililopo Kawe Makuti linaloongozwa na mtume Onesmo Ndegi sambamba na kusindikizwa na waimbaji kama Elly Jo, John Honore, Heleni Kijazi (mwimbaji wa taarabu), Bombi Johnson na wengineo.
Waimbaji hao wanatarajia kuachia album yao mwezi Juni mwaka huu, ikiwa na nyimbo kama Alipokuja Yesu, Wewe ni Mwema, Mungu wa Namna Hiyo, Yale Yametenda na nyinginezo.
(Na Gabriel Ng’osha-GPL)
Hongera sana team SMG. Ilikuwa nzuri sana
safi sana