The House of Favourite Newspapers

Biashara United Yamaliza Biashara na Majembe ya Kazi

0

BIASHARA United wanaopenda kujiita Wanajeshi wa Mpakani wameanza kazi ya kutambulisha majembe mapya kwa ajili ya msimu ujao wa 2021/22.

 

Timu hiyo iliwatema nyota wao17 ambao walikuwa nao msimu uliopita na kuwatakia kila la kheri itashiriki mashindano ya kimataifa katika Kombe la Shirikisho.

 

Miongoni mwa nyota ambao wametambulishwa ni pamoja na Kassim Mdoe kutoka Tanzania Prisons ametua mikononi mwa ‘Wanajeshi wa Mpakani’, Biashara United kwa dili la miaka miwili.

 

Jana Agosti 10 ilimtambulisha Aniseth Revocatus kutoka Mwadui FC, Toyo Odongo Matthew kutoka Zoo United ya Kenya.

 

Agosti 9 ilimtambulisha nyota Atupele Green Jakscon.Kwa mujibu wa uongozi wa Biashara United umeweka wazi kwamba usajili umekamilika kilichobaki ni muda wa kuwatambulisha wachezaji wao.

Leave A Reply