The House of Favourite Newspapers

BIFU ZITO: HARMONIZE AANIKA MAPYA YA WOLPER, SHAMSA AMVAA

MSANII wa Bongo Fleva, Harmonize ‘Konde Boy’ ameibuka na mpya huku vita baridi kati yake na ex girlfriend wake ambaye ni Staa wa Filamu nchini, Jacqueline Wolper ikizidi kushika kasi kwenye mitandao ya kijamii.
Kufuatia taarifa zilizopo kwenye mitandao ya kijamii ambapo Wolper ameonekana akitupia madongo heavy Sarah ambaye ni mpenzi wa Harmonize kwa kumuita eti ni ‘Mlezi wa Wana’ kufuatia tsarifa kusambaa kuwa Mzungu huyo kamkacha Harmonize na kuchepukia kwa bodigadi wa Diamond, Mwarabu Fighter.
Sinema la wana likaendelea huku Harmonize akitokwa na povu la OMO kupitia Instagram aambapo alimtetea mpenzi wake Sarah na kusema yeye sio Mlezi wa wana bali Wolper ndo Mlezi wa Wana na kuambatanisha orodha ya wanaume wote aliokuwa nao Kwenye Mahusiano akiwemo mume wa Shamsa Ford, Chid Mapenzi.
Povu la Shamsa baada ya mume wake, Chid Mapenzi kutajwa kubanjuka na Wolper.

Comments are closed.