Boko Haram Waua Wakulima 43 Nigeria
Kundi la Boko Haram la Nchini Nigeria limewaua Wakulima 43 wa Jimbo la Borno katika mashamba yao ya mpunga yaliopo Zabrmari
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari kupitia Ukurasa wake wa Twitter ameonesha kusikitishwa na kitendo hicho, pia amelaani mauaji hayo. Amesema kuwa, Serikali ya Nigeria imefanya yote yanayowezekana kulinda nchi hiyo na watu wake.
Aidha, Shirika la Kimataifa La kutetea Haki za Binaadamu, Amnesty International limelaani kitendo hicho.
Boko Haram mara kwa mara wamekuwa wakifanya mashambulizi kwa raia ikiwa sehemu ya kushinikiza kuachiwa wajitawale Kaskani mwa Taifa hilo.