The House of Favourite Newspapers

Wapinzani wa Simba Waliwahi Kushinda 79-0, Wakafungiwa

0

 

LIGI ya Mabingwa Afrika inatarajiwa kuanza wikiendi hii, ni michuano ya 25 tangu kuanzishwa kwa mfumo wa ligi hiyo unaotumika kwa sasa.

 

Simba ni timu pekee kutoka Tanzania Bara inayoshiriki katika michuano hiyo, huku Zanzibar ikiwakilishwa na Mlandege katika michuano hiyo.

 

Simba ambao waliondoka nchini Jumanne hii, wanatarajiwa kukipiga dhidi ya Plateau United FC ya Nigeria katika Hatua ya Awali.

 

Wapinzani hao wa Simba ni timu ya muda mrefu lakini katika michuano na ligi ngazi ya juu haina rekodi kubwa kama ilivyo kwa wababe hao wa Msimbazi.

 

Plateau United FC Kuanzishwa:    1975 Uwanja: New Jos Idadi ya siti:      40,000 Makazi: Jos, Nigeria Mwenyekiti: Pius Henwan Meneja: Abdu Maikaba Jezi ya nyumbani: Njano Jezi ya ugenini: Kijani Jezi ya tatu: Nyeupe

 

 

Jina kamili la timu hii ni Plateau United Football Club lakini kwa ufupi inajulikana kwa jina la Plateau United. Kabla ya mwaka 1991 ilikuwa ikijulikana kwa jina la JIB Strikers FC.

Taji lao la kwanza kubwa walilipata mwaka 1999, hiyo ni baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Iwuanyanwu Nationale katika Nigerian Cup.

 

Mara yao ya kwanza kushiriki katika michuano ya Afrika ilikuwa mwaka 2000, lakini waliondolewa mapema tu katika hatua ya awali.

 

Baada ya hapo walipotea na kurejea katika Nigeria Premier League kwa mara ya kwanza msimu wa mwaka 2010/11, bahati mbaya walishuka daraja mwaka mmoja baada ya kupanda.

 

Mwaka 2015 walirejea katika ligi kuu hiyo baada ya kufanikiwa kupata pointi siku ya mwisho ya msimu husika.

Skendo nzito

Mwaka 2013, timu yao ya pili yaani ambayo mara nyingi inatumika kukuza wachezaji ambao baadaye wanapelekwa kikosi cha kwanza ikiwa watafanya vizuri, iliingia katika skendo nzito ya upangaji matokeo nchini Nigeria.

 

Timu hiyo iliyojulikana kwa jina la Plateau United Feeders ilishinda kwa mabao 79-0 dhidi ya Akurba FC, siku ya mwisho ya msimu ambapo walitakiwa kupanda daraja, huku matokeo ya upande wa pili ambayo nayo yalihusisha wapinzani wao waliokuwa wakiwania nao kupanda daraja wakipata matokeo ya ajabu.

 

Ilikuwa Julai 22, 2013, ambapo upande wa pili mchezo uliokuwa ukichezwa pamoja na huo wa Plateau, timu ya Police Machine FC ilishinda mabao 67 dhidi ya Bubayaro FC.

Kabla ya michezo hiyo miwili, Plateau United Feeders na Police Machine ziliingia uwanjani zikiwa zinalingana pointi, ushindi na wastani mzuri wa mabao ungeipa timu moja nafasi ya kupanda daraja.

 

Hadi kipindi cha kwanza Plateau ilikuwa ikiongoza 7-0, kipindi cha pili ikaongeza mabao 72 huku Police Machine wao walikuwa wakiongoza 6-0 hadi mapumziko, kipindi cha pili wakafunga mabao 61.

 

Kwa matokeo hayo, Plateau wakawa na nafasi ya kupanda kwa kuwa walikuwa na wastani mzuri wa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa dhidi ya Police Machine.

 

Kwa matokeo hayo, timu hizo zote zilizohusika katika upangaji matokeo ambazo ni Plateau Feeders, Akurba FC, Police Machine FC na Bubayaro FC zote zilifungiwa kwa muda wa miaka 10 huku wachezaji na maofisa walioshiriki na kuhusika katika kupanga matokeo nao wakifungiwa maisha kutojihusisha na mchezo wa soka.

 

Ubingwa mmoja tu

Plateau United ilifanikiwa kubeba ubingwa wa Ligi Kuu ya Nigeria kwa mara ya kwanza na pekee mwaka 2017, ikiwa chini ya Kocha Kennedy Boboye.

 

Walivyopata uwakilishi Caf

Inaweza kukushangaza kuona wamebeba ubingwa mara moja tu mwaka 2017 lakini msimu huu wanaiwakilisha Nigeria katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

 

Ipo hivi, wakati msimu uliopita wa 2019/20 ukiendelea, ndipo kulipoibuka janga la maambukizi ya Virusi vya Corona, ligi nyingi zilisimama ikiwemo ya nchi hiyo.

 

 

Mamlaka husika wakashindwa kuirejesha ligi hiyo na kuamua kuipa ubingwa timu iliyokuwa kileleni ambayo ni Plateau United. Hivyo, siyo mabingwa kama ilivyo kwa Simba ambao walibeba ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania.

 

Ilifukuza wachezaji 9 kwa mkupuo

Mbali na skendo hiyo, pia Plateau United FC hii yenyewe sasa ya wakubwa iliwahi kufukuza wachezaji tisa kwa wakati mmoja katika kile walichosema ni kuiokoa timu hiyo isishuke daraja katika Ligi Kuu ya Nigeria mwaka 2011.

Kulikuwa na sababu mbalimbali za kuwafukuza wachezaji hao ikiwemo utoro, nidhamu, kiwango duni na kutowajibika katika majukumu.

Wachezaji waliowahi kuichezea timu hiyo na kufanikiwa:

John Obi Mikel

Umri: 33

Nafasi: Kiungo mkabaji

Timu vijana:

2002-2004        Plateau United

 

Timu za wakubwa

2004-2006        Lyn

2006-2017        Chelsea

2017-2018        Tianjin TEDA

2019                   Middlesbrough

2019-2020        Trabzonspor

2020-sasa         Stoke City

 

Nigeria

2005-2019

Mechi 91

Mabao 6

 

Chris Obodo

Umri: Miaka 36

Nafasi: Kiungo mkabaji

 

Timu ya vijana:

Plateau United

 

Tumu za wakubwa

2001-2004        Perugia

2004-2005        Fiorentina

2005-2012        Udinese

2010-2011        →     Torino (mkopo)

2011-2012        →     Lecce (mkopo)

2013                   Dinamo Minsk

2014                   Olhanense

2014–2016       Skoda Xanthi

2016                   Concordia Chiajna

2016                   Pandurii Târgu Jiu

2017                   Apollon Smyrnis

 

Nigeria

2004-2008

Mechi 21

Mabao 4

 

 

Celestine Babayaro

Umri: Miaka 42

Nafasi: Beki wa kushoto

 

Timu ya vijana

1994          Plateau United

 

Timu za wakubwa

1994-1997        Anderlecht

1997-2005        Chelsea

2005-2008        Newcastle United

2008          LA Galaxy

 

Nigeria

1995-2004

Mechi 27

Mabao 0

Victor Obinna

Umri: Miaka 33

Nafasi: Straika

 

Timu za vijana

2003          Plateau United

2004          Kwara United

2005          Enyimba

2005          Internacional

 

Timu za wakubwa

2005-2008        Chievo

2008-2011        Internazionale

2009-2010        → Málaga (mkopo)

2010-2011        → West Ham United (mkopo)

2011-2015        Lokomotiv Moscow

2014          → Chievo (mkopo)

2015-2016        MSV Duisburg

2016-2017        Darmstadt 98

2017-2018        Cape Town City

 

Nigeria

2005-2014

Mechi 48

Mabao 12

 

Shehu Abdullahi

Umri: Miaka 27

Nafasi: Kiungo

 

Timu ya vijana

2011          Plateau United

 

Timu za wakubwa

2012–2014       Kano Pillars

2014–2015       Qadsia

2015–2016       União da Madeira

2016–2018       Anorthosis

2018–2020       Bursaspor

2020–       Omonia

 

Nigeria

2014-sasa

Mechi 31

Mabao 0

John Joseph na mtandao

 

 

 

 

 

 

Leave A Reply