The House of Favourite Newspapers

Bosi wa Manchester City Pep Guardiola Awaonya Real Madrid

0
Bosi wa Manchester City, Pep Guardiola.

BOSI wa Manchester City, Pep Guardiola amewaonya Real Madrid kuwa makini kwani ameanza kuwafukuzia katika kutwaa mataji ya UEFA.

Hii ni baada ya wikiendi iliyopita Manchester City kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza.

Guardiola aliiongoza Man City kutwaa taji la kwanza la UEFA katika historia ya klabu hiyo, lakini yeye kama kocha akitwaa kwa mara ya tatu baada ya huko nyuma kutwaa akiwa na Barcelona.

Katika historia ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Real Madrid ndiyo baba lao wakiwa wametwaa mataji hayo mara 14 ikizifunika klabu zote.

Guardiola alisema Madrid wanatakiwa kuwa makini kwani bado mataji 13 tu aweze kuwafikia.

Bosi huyo alinukuliwa akisema: “Real Madrid wanatakiwa kuwa makini, tupo nyuma kwa mataji 13, wanatakiwa kujua kwamba wakizubaa sisi tunakuja taratibu, tutawafikia.”

YANGA YAMALIZA KIBABE, MAYELE, SAIDO KIMEELEWEKA/ SIMBA YAMFICHA KIUNGO MCAMEROON DAR…

Leave A Reply