Breaking: Mangula Ajiuzulu, Kinana Atangazwa Kumrithi -Video
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Philip Mangula leo Alhamisi Machi 31, 2022 amewasilisha katika Halmashauri Kuu ya CCM barua ya kuachia nafasi hiyo.
Halmashauri kuu pia imemteua Abdulrahman Kinana kuwa mgombea wa nafasi hiyo ambapo jina lake litapigiwa kura hapo kesho kwenye mkutano mkuu wa CCM.