The House of Favourite Newspapers

Breaking: Mdee, Bulaya, Meya Jacob Wakamatwa Tena Segerea

0

WABUNGE wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Halima Mdee na Ester Bulaya, Meya wa Ubungo, Boniface Jacob, Katibu wa chama hicho Mkoa wa Dar, Henry Kileo na wafuasi wengine wa chama hicho, wamekamatwa na polisi baada ya kutokea vurugu wakati wakifuatilia kuachiwa kwa Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kutoka Gereza Kuu la Segerea, leo Ijumaa, Machi 13, 2020.

 

Askari Magereza wametumia silaha za moto na kufyatua risasi hewani kuwatawanya wafuasi wa chama hicho waliokuwa nje ya gereza hilo kumsubiri Mbowe akiachiwa huku baadhi ya viongozi na wananchi kadhaa wamejeruhiwa, akiwemo dereva mmoja wa bodaboda ambaye inadaiwa amevunjika mguu.

Mdee na Bulaya waliotoka jela jana baada ya kulipa faini, leo walikwenda kumpokea Mbowe ambaye amekamilisha taratibu za kutoka jela. Viongozi hao wamekamatwa saa 7:30 mchana baada ya kufika katika gereza hilo na kuanza kuzuiwa na askari wa Jeshi la Magereza waliotumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa chama hicho.

Wakati mabomu hayo yakipigwa, viongozi hao wa Chadema waliwekwa chini ya ulinzi kwa madai ya kukiuka amri halali ya kuwataka kuondoka katika eneo hilo. Hata hivyo, Mbowe naye ameachiwa leo baada ya kulipa faini ya Tsh milioni 70 aliyohukumiwa yeye na wenzake tisa na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Jumanne wiki hii.

Leave A Reply