GHOROFA la Upanga mali ya Kampuni ya Lugumi Enterprises Limited limenunuliwa leo (Septemba 9) na kampuni ya Al- Naeen Enterprises kwa Sh700 milioni. Jengo hilo kubwa ambalo limepata mteja lipo maeneo ya Upanga.
Kampuni ya Udalali ya Yono ndiyo inayosimamia mnada wa maghorofa hayo majengo mengine mawili yamekosa wateja kutokana na bei zake kuwa juu ukilinganisha na ukubwa wa jengo.
Akizungumza wakati wa Mnada huo Mkurugenzi wa Kampuni ya Yono Scolastica Kevela amesema nyumba ambazo zimekosa wateja zinauzwa kwa Shilingi 460 milioni ambazo zipo Mbweni JKT.