The House of Favourite Newspapers

Breaking News: Kamati ya Saa 72 Yaipa Simba Pointi 3

0

KLABU ya Simba imezidi kujihakikishia ubingwa wa Ligi Kuu Bara baada ya kushinda rufaa yake dhidi ya Kagera Sugar ambao imethibitika mbele ya Kamati ya Saa 72 kuwa mchezaji wa Kagera Sugar, Mohamed Fakhi alicheza mechi ya Simba akiwa na kadi tatu.

Simba ilikata rufaa ikitaka ipewe pointi tatu kwa kuwa Kagera Sugar ilimchezesha Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano. Katika mechi hiyo, Simba ililala kwa mabao 2-1 na baada ya hapo, ikatangaza kutangaza kukata rufaa.
Kulingana na kanuni za TFF, Kamati hiyo imeipa Simba point zake 3 na magoli mawili baada ya kushinda rufaa yao hiyo dhidi ya Kagera Sugar. Simba imefikisha pointi 61 mbele ya wapinzani wao Yanga wenye Pointi 56.
Leave A Reply