The House of Favourite Newspapers

British Council yakabidhi mpango wa kufundisha Kiingereza

0

1

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dk. Leonard Akwilapo, akizungumza jambo katika hafla hiyo.

2

Shughuli zikiendelea.

3

Kutoka kushoto ni mdau wa elimu kutoka British Council, Richard Sunderland, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo na Kamishna wa Elimu, Dk. Edicorp Shirima.

4Baadhi ya walimu wa shule za sekondari hapa nchini waliohudhuria hafla hiyo.

5

Wadau wa elimu wakifuatilia hafla hiyo.

6

Kitengo cha Tehama kikiwa kazini.

7

Waratibu wa mpango huo wakizungumza jambo.

8

Wadau wa elimu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika hafla hiyo.

9.

Wadau wakiendelea na shughuli mbalimbali.

  SHIRIKA la Misaada la Uingereza lijulikanalo kama British Council jana limekabidhi mpango wa  kuimarisha ufundishaji wa lugha ya  Kiingereza katika shule za sekondari  hapa nchini.
Mpango huo umekamilika  na kukabidhiwa kwa Wizara ya Elimu,  Sayansi na Teknolojia kwa Naibu  Katibu Mkuu Dk. Leonard Akwilapo jana katika Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo,  Akwilapo alisema kuwa  mpango huo ulifanyika kwa majaribio ambapo mikoa mitano ya Tanzania Bara  ilihusishwa,  ambayo ni, Dar es Salaam, Mbeya, Pwani, Kagera na Arusha.
Alifafanua kuwa  mpango  huo umewawezesha wanafunzi wa kidato cha kwanza  kila wanapotoka  shule za msingi kupata masomo ya awali ya lugha ya Kiingereza  kwa muda wa miezi sita.

Aliongeza kuwa  lugha ya  Kiingereza ni daraja linalounganisha ulimwengu  japokuwa  sera ya elimu ya mwaka 2014 inatambua lugha ya Kiswahili na Kiingereza  kuwa ni lugha za kufundishia  kwa ngazi zote kuanzia chini  hadi chuo kikuu  huku lugha ya Kiswahili ikiendelea  kuwa lugha ya kufundishia shule za msingi kama sera inavyoeleza.

Aidha mratibu wa mradi huo, Naomi Swai,  amesema kuwa mpango huo umeleta mafanikio makubwa kwa kuwapatia waalimu  mafunzo ya kufundisha  lugha hiyo na kupata vitabu  vitakavyosaidia njia za kufundishia  Kiingereza ambapo zaidi ya walimu 2,485 na wanafunzi 65,000 wamefanikiwa katika mpango huo kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013.

Na Denis Mtima/Gpl.

Leave A Reply