The House of Favourite Newspapers

Bunge la Ukraine Lapiga Marufuku Kupigwa Muziki wa Wasanii Kutoka Urusi

0
Jengo la Bunge la Ukraine

BUNGE la Ukraine limepiga marufuku kura kwa ajili ya kuidhinisha muswada wa kupiga marufuku muziki wa Kirusi katika maeneo ya umma na kwenye vyombo vya habari.

Aidha, bunge hilo limetoa upendeleo mkubwa wa muziki wa nyumbani yaani Ukraine kwenye vituo vya redio na Televisheni.

Sheria hii inakataza uigizaji wa umma na utangazaji wa kazi ikiwemo video za muziki na wasanii ambao walikuwa  wana uraia wa Urusi baada ya mwaka 1991.

 

Bunge hilo limesema makampuni ya Televisheni na Redio yatakayokiuka kanuni hii yatatakiwa kulipa faini ya 10% ya ada ya leseni.

Licha ya adhabu hiyo kutolewa lakini haitaathiri kazi za wasanii ambao walilaani uvamizi wa kijeshi wa Urusi dhidi ya Ukraine.

Muswada huo unahitaji wasanii wenye nia au wawakilishi wao kwa ajili ya kuwasilisha maombi katika fomu iliyowekwa kwa huduma ya usalama ya Ukraine (SBU).

Hivyo, wasanii hao watalazimika kusaini tamko la kulaani uvamizi wa Urusi na kutaka vita hivyo vikomeshwe mara moja.

Leave A Reply