WAFUASI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), leo wamefurika katika viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar wakiimba nyimbo za kutaka Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe na viongozi wenzake waachiwe.
Mbowe na wenzake ambao ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Vincent Mashinji na manaibu wake wa Bara na Zanzibar, John Mnyika na Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko wote wanakabiliwa na mashtaka manane yakiwemo mawili ya uchochezi wa uasi yanayomkabili Mbowe na wanatarajiwa kuachiwa kwa dhamana leo.
Wafuasi hao wamekuwa mahakamani hapo tangu mapema asubuhi leo wakisubiri kuwalaki viongozi hao waliokaa rumande kwa siku saba tangu wiki iliyopita.
UPDATES: Viongozi wa Chadema wakiongozwa na Freeman Mbowe wametimiza masharti ya dhamana katika kesi yao Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Aidha, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi ameomba kufanya marekebisho ya hati ya mashtaka ili kumjumuisha Mdee katika kesi inayowakabili viongozi wengine sita wa Chadema.
Comments are closed.