Chege: Sijawahi kuwa na bifu na Nature
Chegge Chigunda.
Chegge wa Kwanza Kushoto na watatu ni Juma Kassim ‘Nature’ wakiwa na wadau wa muziki
NYOTA wa Bongo Fleva aliyefanya vyema kibao cha Waache Waoane, Said Juma ‘Chege’ amefungukia madai ya kuwa na bifu kwa muda mrefu na Juma Kassim ‘Nature’, akisema madai hayo hayana ukweli.
Juma Nature.
Chegge na Temba.
Akichonga na Risasi Vibes, kupitia Global TV Online, Chege ambaye aliongozwa na Nature wakiwa TMK Wanaume Family kabla ya kundi hilo kugawanyika, alikiri kuwa anaonana na Nature kwa nadra kutokana na changamoto za kimaisha kwani kila mmoja yupo bize kivyake.
“Mimi sina bifu na Nature, tupo vizuri kabisa, sema hatufanyi kazi pamoja, wala kukutana kwa sababu ya changa-moto za kimaisha, lakini sina tofauti naye kabisa,” alisema Chege.
Kutazama mahojiano zaidi, ingia www.globaltvtz.com
Comments are closed.