The House of Favourite Newspapers

Chemsha Bongo ya Gazeti la Ijumaa Yashika Kasi Kitaa

0
Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Anthon Adam ( wa pili kulia mwenye fulana ya Ijumaa Nyeusi) akipozi na wasomaji wa gazeti la Ijumaa baada ya kuwakabidhi zawadi zao.

IKIWA ni wiki moja baada ya kuzinduliwa kwa Chemshabongo na Gazeti la Ijumaa ambap msomaji wa gazeti hilo hujibu maswali kwa ufasaha kupitia ukurasa wa pili ndani ya gazeti hilo, leo wasomaji wameanza kujinyakulia zawadi hizo nono kutoka Gazeti hilo.

Ofisa masoko wa Kampuni ya Global Group, Songoro Bilal (kushoto) akimkabidhi fulana mwanamama aliyekutwa akilisoma gazeti la Ijumaa kama zawadi zinazotolewa na kampuni hiyo.

 

Timu ya Masoko na Usambazaji ya Global Publishers ilikuwa mtaani ikimwaga zawadi hizo zikiwemo fulana huku wasomaji wengine wakirudishiwa kiasi cha pesa walichonunulia gazeti hilo katika maeneo ya Mabibo, Manzese na Mburahati jijini Dar es Salaam ambako kote ilikopita imeweza kuwazawadia zawadi wasomaji hao waliokutwa wakilisoma gazeti hilo.

 

Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Anthon Adam ( kushoto) akimkabidhi fulana msomaji wa Ijumaa.

 

Aidha, msomaji anachotakiwa ili kujinyakulia fedha Taslimu Tsh. 30,00 au fulana nikununua gazeti la Ijumaa kisha kujibu kwa ufasaha swali la chemshabongo iliyopo kwenye ukurasa wa pili na kutuma kwa namba ya maalum iliyopo  kwenye ukurasa huo.

Msomaji akisoma gazeti la Ijumaa kabla ya kupatiwa zawadi yake.

 

Baada ya kuhamishia mitandaoni pekee magazeti mengine ya Udaku ya Global Publishers, Ijumaa ndiyo Gazeti pekee la Burudani nchini Tanzania linalopatikana mtaani kwa sasa ambalo limeboreshwa kuanzia stori, upambaji wa kurasa, makala, machombezo na hadithi za mtunzi mahiri, Eric Shigongo.

 

Ofisa masoko wa Kampuni ya Global Group, Songoro Bilal (kushoto) akimrudishia msomaji wa Gazeti la Ijumaa fedha aliyonunulia baada ya kukutwa akilisoma gazeti hilo kama zawadi zinazotolewa na kampuni hiyo.

 

Pia kuna kolamu zote kali zilizokuwa kwenye magazeti mengine Udaku ili kukufanya usi-miss kitu hata kimoja cha udaku iwe ndani ama nje ya Tanzania.

 

Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Anthon Adam (wa kwanza kushoto)akiwaelekeza wasomaji wa gazeti la ijumaa waliokutwa wakilisoma namna ya kujaza sehemu ya chemshabongo ilipo katika gazeti hilo.

 

Nunua Gazeti la Ijumaa kila Ijumaa linapokuwa mtaani ili upate uhondo, si hivyo tu bali pia utapata zawadi za kutosha.

 

Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Anthon Adam (kulia) akimwonesha msomaji wa gazeti la Ijumaa ukurasa wenye chemshabongo ambayo wasomaji wake wanajaza na kuibua na fedha taslimu Tsh.30,000 au fulana pale wanaposhinda.

 

Ofisa masoko wa Kampuni ya Global Group, Songoro Bilal (kushoto) akiwaelekeza jambo wasomaji wa Gazeti la Ijumaa juu ya kushiriki kujaza chemshabongo inayopatikana ndani ya gazeti hilo.

 

 

 

 

 

Leave A Reply