Chid Benz: Bongo Fleva Inakwenda Mbali
MSANII wa Muziki wa Kizazi Kipya, Bongo Fleva, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’, amesema kuwa muziki huo kwa sasa unaonekana utafika mbali zaidi kutokana na jinsi wasanii wanavyojituma kila kukicha tofauti na zamani.
Chid ambaye amewahi kuwika na nyimbo kibao zikiwemo Dar es Salaam Stand Up, Mmenisoma, Naitwa Nani aliomshirikisha K-Lyin na Hasira za Nini, amesema kuwa, muziki wa Bongo Fleva unapiga hatua siku hadi siku kutokana na wasanii wanavyojituma, hivyo utafika mbali zaidi.
“Muziki wa Bongo Fleva unaweza kufika mbali zaidi kwa kuwa wasanii wanaonekana kujituma zaidi, kila siku kinakuja kitu kipya, wanaonyesha uwezo mzuri wa kuhitaji kufika mbali,” alisema Chid Benz alipozungumza na Kilinge juzi Jumamosi.
Khadija Mngwai, Dar es Salaam.
Comments are closed.