Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo yupo Mkoani Iringa kwa ziara ya siku saba kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM, kuhamasisha uhai wa Chama ngazi za mashina pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi, huku maagizo mbalimbali anayotoa yakiendelea kutekelezwa.
Katibu Mkuu huyo ameambatana na wajumbe wawili wa sekretarieti ya CCM Taifa, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema na Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Haji Ussi Gavu.