The House of Favourite Newspapers

Chris Brown: Sivuti Sigara Karibu na Mwanangu

0

rs_634x1024-150517182311-634.chris-brown-baby-royalty-Billboard-Awards.jl.051715 Chris Brown na mwanaye, Royalty

Tamthiliya inaendelea kati ya Chris Brown na mama wa mtoto wake, Nia Guzman.

Mwishoni mwa wiki jana, Guzman alikaririwa akisema kuwa, Chris aekuwa akivuta sigara karibu na mazingira alipo mtoto wao huyo, hivyo kumsbabishia mtoto ugonjwa wa pumu (asthma).

The-Source_Chris-Brown-x-Nia-GuzmanChris Brown, mama wa mtoto wake, Nia Guzman na Royalty.

Kwa upande wake Chris akikanusha madai hayo ya mzaiz mwenzake kwa kuandika kwenye mtandao wa Instagram kuwa hawezi kufanaya upuuzi kama huo.

“Nilishaacha uvutaji wa sigara tangu kitambo,” aliandika hivyo. “Hakuna mtu yeyote anavuta sigara karibu na mwanangu… Ninajari na kumthamini mwanangu na siwezi kumuweka kwenye mazingira ambayo yatamdhuru.”

#chrisbrown denies #tmz story about him causing his daughter to have asthma

A photo posted by DJ Akademiks (@iamakademiks) on


Brown aliongeza kuwa, madai ya mzazi mwenzake ilikuwa anataka apewe pesa ili aongeze kipato chake. Kulingana na ripoti ya jarida la TMZ, Guzman anahitaji pesa kiasi cha dola za Marekani 16,000 kila mwezi kwa ajili ya atuizi ya mtoto, ikiwa ni ongezeko kubwa kutoka kiasi cha dola za Marekani 2,500 anazopewa kwa sasa kulinagana na makubaliano.

chris-brown-little-more-music-video-with-daughter-royaltyOktoba mwaka jana, Guzman na Brown walikubaliana kuchangia atumizi ya mtoto wao na Desemba, Brown aliachia albamu yake mpya aliyoiita jina la mwanaye Royalty.

Leave A Reply