The House of Favourite Newspapers

Coastal Yafafanua Usajili Wa Alikiba

Mwanamuziki maarufu nchini, Ali Saleh Kiba ‘Alikiba’

 

BAADA ya Coastal Union kufanikiwa kumpa mkataba wa mwaka mmoja mwanamuziki maarufu nchini, Ali Saleh Kiba ‘Alikiba’, uongozi wa timu hiyo umesema hautamzuia kufanya kazi yake ya kuimba.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, meneja wa timu hiyo, Said Hilary alisema Ali Kiba ni mchezaji mzuri na ameenda kwenye timu ya mpira na lengo lao kubwa ni kuitangaza Coastal.

 

“Tumemsajili kwa mkataba wa mwaka mmoja na tunafahamu yeye ni mwanamuziki kwa hiyo akiwa na shughuli zake za kimuziki ataendelea na shughuli zake kama kawaida na akiwa yupo huru basi atacheza kuisaidia timu maana tuna uamini uwezo wake ndiyo maana tumemsajili,” alisema Hilary.

Na Isaya Mbena, Championi Ijumaa

Comments are closed.