MKURUGENZI Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, amesema benki hiyo imeamua kuongeza kiwango cha mkopo kutoka Milioni 50 hadi 100 na pia wameshusha kiwango cha riba kwa wateja wao watakaochukua mkopo ili kuwawezesha kutimiza malengo yao ikiwa ni pamoja na kufungua biashara na vingine vingi.
Mbali na hayo, Dkt Mimeo amesema iwapo mtu atawasilisha nyaraka zote muhimu wakati wa kuomba mkopo atapewa ndani ya saa 24 huku muda wa kurejesha mkopo huo kutoka miaka mitano hadi miaka saba.
Comments are closed.