The House of Favourite Newspapers

Cristiano Ronaldo Aanza Harakati za Kurejea Man U

STAA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo hana furaha Real Madrid na anataka kurejea Manchester United. Ronaldo amekasirishwa na kitendo cha uongozi wa klabu hiyo kushindwa kuzungumza naye ili kuongeza mkataba wake.

 

Kwa mujibu wa magazeti ya Hispania ni kuwa Rais wa klabu hiyo, Florentino Perez alimwahidi kumwongeza mshahara mapema lakini ameshindwa kutimiza ahadi yake.

 

Ronaldo amehuzunishwa kujikuta kuwa yupo nje ya listi ya wachezaji watatu nyota duniani wanaopata mishahara mikubwa. Mwanasoka huyo bora wa dunia mara tano, anapata kiasi cha pauni milioni 19 kwa mwaka.

 

Kufuatia hali hiyo, nyota huyo ameuambia uongozi wa Real Madrid anataka kuondoka mwishoni mwa msimu huu. Hata hivyo, mreno huyo msimu huu amekuwa na kiwango kibovu, ambapo amefunga mabao manne tu.

MADRID, Hispania.

Comments are closed.