CUF Kutoa tamko kuhusu kurudiwa uchaguzi Zanzibar
Katibu Mkuu wake, Maalim Seif Sharif Hamad.
Wakati hatima ya CUF kushiriki au kutoshiriki uchaguzi wa marudio inatarajia kufahamika leo, mgawanyiko mkubwa umeibuka miongoni mwa wajumbe wake wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa.
Akizungumzia mgawanyiko huo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa CUF, Ismail Jussa Ladhu, alisema kutokana na ukubwa na uzito wa mgogoro wa uchaguzi, mgawanyiko ni jambo ambalo halikwepeki kwa chama kikubwa kama hicho.