Dar Waadhimisha Uhuru kwa Kufanya Usafi
Wafanyakazi wa Manispa ya Kinondoni kwa kushirikiana na polisi wa Osyterbay wakifanya usafi maeneo ya Bamaga-Mwenge.
RPC wa Wilaya ya Kinondoni, Camilius Wambura, (katikati) akiwa na baadhi ya vijana wa ‘Dar Laning Club’ ya Kinondoni kufanya usafi kwenye maeneo ya kituo cha daladala cha ITV kutokea maeneo ya Bamaga.…Wakizoa takataka eneo la kituo cha daladala cha ITVRPC Wambura (Kushoto) akiendelea kufanya usafi.Barabara ya Bamaga-Mwenge ilivyoonekana mara baada ya kufanyiwa usafi.Zoezi la usafi likiendelea.Wafanyakazi wa Hospitali ya Kijitonyama wakifanya usafi kwenye hospitali yao.
Zoezi likiwa limepamba moto.
Polisi wa Kijitonyama ‘Mabatini’ wakifanya usafi katika maeneo yao.Kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ ikionekana kuungwa mkono na askari hao.Hapa ni usafi tu. Akina mama wa kikundi cha Vikoba Endelevu wakiungana na polisi wa Kijitonyama kufanya usafi maeneo ya kituoni hapo.
WAKAZI wa jijini Dar es Salaam, hii leo wemeadhimisha siku ya mika 54 ya uhuru kwa kufanya usafi katika mitaa mbalimbali ya huku viongozi wa serikali na taasisi wakishirikiana na wananchi kusafisha mazingira kwa kauli mbinu ya ‘Hapa Ni Usafi Tu’.
Zoezi hilo limefikia kilele hii leo tokea tamko la Rais John Pombe Magufuli kuwataka wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao ili kuondokana na magonjwa ya mlipuko kikiwemo kipindupindu.
Kamera ya GPL imepita maeneo mbalimbali ya Mwenge, Bamaga, Hospitali ya Kijitonyama na katika kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’ na kukuta usafi ukiendelea.
NA DENIS MTIMA/GPL