The House of Favourite Newspapers

DARASA AONYESHA JEURI YA PESA

WAKATI mta­zamo wa baadhi ya watu wakiamini kuwa Muziki wa Hip Hop Bongo haulipi kivile, hali imekuwa tofauti kwa staa Sharif Thabeet ‘Darassa’ baa­da ya kubainika anaishi kwenye mjengo wa kifahari uliopo maeneo ya Bahari Beach jijini Dar. 

 

 Tangu atambe na Wimbo wa Muziki miaka miwili iliyopita kisha akaachia Wimbo wa Hasara Roho, Darassa hakuonekana tena kwenye ulingo wa muziki hali iliyozua sinto­fahamu kwa mashabiki wake.

 

ALIUNDIWA ZENGWE

Baada ya kujificha kwa zaidi ya mwaka, mwishoni mwa mwaka jana zilivuja taarifa kuwa msanii huyo amejiingiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya ambapo gazeti dugu na hili la Ijumaa lili­chimba na kubaini haikuwa kweli.

 

TUPATE HABARI MPYA

Mwishoni mwa wiki iliyopita, mapa­parazi wetu wa kitengo maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) walipenyezewa ubuyu mpya wa mjini kuwa msanii huyo kwa sasa maisha yake yamenyooka na kwamba anaishi kwenye jumba la kifahari na magari mawili ya kutem­belea akiwa na mke wake, mtoto mmoja wa kike pamoja na mama yake mzazi.

 

“Natumai hapo ni kikosi kazi cha OFM, watu wanasema tu kuwa ohhh Hip Hop hailipi kwamba wanaofanikiwa kumiliki ma­jumba ya kifahari ni wa kuimba kama vile Kiba (Ally Salehe) na Diamond (Nasibu Abdul), hivi mmeona maisha ya Darassa anayoishi kwa sasa? Mmeona hayo magari yake? Fanyieni kazi yupo Bahari Beach huku njooni,” kilisema chanzo.

OFM KAZINI

Baada ya taarifa hizo kutua dawatini, OFM ilifuata ramani iliyoelekezwa hatua kwa hatua hadi katika mjengo huo ambapo baada ya kufika getini, waliku­tana na dada wa kazi katika nyumba hiyo ambaye hakujitam­bulisha jina.

“Karibuni ndani, karibuni sana!”

 

MANDINGA YAMEPAKI NJE

Mara baada ya kuingia eneo la ndani ya fensi, OFM ilishuhudia mjengo wa kifahari wa ghorofa moja sambamba na magari ya kifahari; BMW jeusi pamoja na Toyota Alphard.

 

MENEJA WAKE AFUNGUKA

Wakiwa bado katika mjengo huo ambao walikaribishwa hadi sebuleni, OFM walipata nafasi ya kuzungumza machache na meneja wa Darassa anayefa­hamika zaidi kwa jina moja la Kimbe.

OFM: Sisi ni waandishi tu­mekuja kufanya mahojiano na Darassa?

 

Meneja: Kwa sasa Darassa amelala, huwa ana kawaida ya kushinda studio kwake kwenye hicho chumba cha pili (anaone­  sha) na ikifika saa moja asubuhi hupumzika. Labda mpange siku nyingine mje kumtembelea. Licha ya kutopata fursa ya kuzungumza na Darassa mwenyewe, OFM iliweza kush­uhudia ndani ya mjengo huo wenye ‘sebule kama uwanja wa taifa’ ukiwa umesheheni samani nzuri na za kuvutia.

 

Ijumaa Wikienda lilitaka kujua zaidi kuhusu mjengo huo wa kifahari kama Darassa amepanga au anamiliki pamoja na maswali mengine lakini meneja wake huyo, aliwataka waandishi wafike siku nyingine wazungumze kila kitu Darassa mwenyewe akiwepo.

ANAMILIKI AU KAPANGA?

Ili kujishibisha zaidi kujua kama kweli anamiliki au amepanga mjengo huo, OFM walitoka moja kwa moja hadi kwa Mjumbe wa Serikali za Mitaa, Athuman Nas­sor ambaye alisema: “Kwanza hizo taarifa za Darassa kuishi maeneo hayo mnayosema ndiyo kwanza nazisikia kutoka kwenu ila kuna mjumbe mwenzangu anayehusi­ka na masuala ya ardhi ngoja nikawakutanishe naye ili aweze kuwasaidia.”

 

OFM walipomfikia mjumbe huyo anayehusika na kitengo cha ardhi, Khalfan Suleiman, naye alifunguka hivi: “Ninachokifahamu hiyo nyumba anamiliki mama mmoja anaishi Kunduchi (mama Maua) ila sina uhakika kama ame­shaipangisha au ameshaiuza kwani sijafika eneo hilo kwa muda mrefu.”

TUJIKUMBUSHE

Kabla ya kutoka kimuziki, Dar­assa alikuwa akiishi na mama yake mzazi maeneo ya Kiwalani jijini Dar na baada ya kuanza kukubalika kupitia Wimbo wa Muziki ambao ulimpatia mafani­kio makubwa, alihamia maeneo ya Makongo Juu na kuchukua nyumba nzima.

Imeandikwa na Stori: Sha­muma Awadhi na Memorise Richard.

Comments are closed.