Na Dustan Shekidele, Global Publishers |Morogoro
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Shahidi Mchembi akiwa viongozi wengine wilayani humo wametembelea Kijiji cha Kisitwi kwa ajili ya kuhimiza maendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Shahidi Mchembi akiwa ofisini kwake.
Tukio hilo limetokea wiki iliyopita wilayani humo ambapo mkuu huyo wa wilaya, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Clement Mjulwa, Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya, Abdi Ndilla na Katibu Tawara wa Wilaya, Adam Bibangaba walifika kijijini hapo na kufanikiwa kuzungumza na wananchi wakihimiza maendeleo, uchapa kazi.
DC Mchembi akipanda kwenye gari lake.
Aidha DC Mchembi alifika katika Shule ya Msingi Kiswiti liliyopo kijijini hapo Kata ya Lubeho umbali wa takribani kilomita 20 kutoka Gairo Mjini na kukabidhi madawati 50 ya msaada yaliyotolewa na Bank ya Exim.
Kabla ya kufika shuleni hapo, msafara huo ulikwama katikati ya msitu kufuatia barabara kukatika na magari kushindwa kupita, hivyo DC Mchembi na msafara wake waliamua kushuka kwenye magari yao na kutembea kwa miguu umbali wa takribani mita 200 ili kuvuka upande wa pili na kuendelea na safari yao.
Miundombinu ya barabara kuelekea Kijiji cha Kiswiti
DC Mchembi akipokelewa shuleni hapo.
Comments are closed.