The House of Favourite Newspapers

DC JOKATE: SINA AKAUNTI YA VIKOBA, MSITAPELIWE!

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, Jokate Mwegelo, akisani kitabu cha wageni baada ya kutembelea Ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori, Dar,  leo.

MKUU wa Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, Jokate Mwegelo, amewataka Watanzania waelewe kwamba hana akaunti yoyote ya vikoba kwenye mitandao ya kijamii ya Instagram au Facebook inayotoa mikopo kwa wananchi.

Akizungumza jana katika Ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori,  Dar,  Jokate amesema kumekuwa na watu ambao wametengeneza akaunti  feki wakijifanya ni yake na kuwatapeli wananchi kwa kuwachangisha kwa maelezo kwamba anatoa mikopo.

Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa, Richard Manyota (kushoto) akiongea jambo na Jokate (kulia). Wengine kutoka kulia (wa pili) ni Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally, akifuatiwa na Mhariri Elvan Stambuli; Meneja Mkuu wa Global Group, Abdallah Mrisho na Mhariri wa gazeti la Championi Jumatatu, Ezekiel Kitula.

“Mimi sina akaunti yoyote ya vikoba na sijihusishi na jambo hilo, kwa vyovyote waliofungua akaunti hiyo kwa jina langu ni matapeli, wana nia ya kuwaibia wananchi,” amesema Jokate.

Mhariri wa gazeti la Amani, Erick Everest, akiMkabidhi Jokate gazeti la Amani.

Akifafanua zaidi, mkuu huyo wa wilaya kijana amesema amekuwa akipokea wageni mbalimbali wengine kutoka mikoani ofisini kwake wakidai kwamba wametuma fedha kwenye akaunti hiyo feki ya vikoba.

Mhariri wa Championi Jumatano, Philip Nkini, akimkabidhi Jokate gazeti la Championi Jumatano.

“Jana tumepokea mtu kutoka Tabora anadai amefuatilia akaunti hiyo feki kwa sababu alituma fedha, niwafahamishe wananchi kwamba sina vikoba mimi na wala sijafungua kwenye akaunti yoyote, iwe kwenye Instagramu au mitandao mingine yeyote,” amesema Jokate na kuwasisitizia wananchi kuwa makini na matapeli hao.

Mhariri wa Championi Ijumaa, John Joseph, akimkabidhi Jokate gazeti la Championi Ijumaa.

Hivi karibuni kumekuwa na mtindo wa matapeli kutumia mitandao ya kijamii kuwaibia wananchi na wengine kutumia simu kufanya uhalifu huo, jambo ambalo jeshi la polisi limekuwa likituma ujumbe kwenye simu za kiganjani kutahadharisha watu kujihadhari na wizi wa aina hiyo.

Mhariri wa Championi Jumatatu akimkabidhi Jokate gazeti la Championi Jumatatu.

Jokate akiwa katika picha na baadhi ya wafanyakazi wa Global Group mwishoni mwa ziara yake.

 

PICHA NA MUSA MATEJA | GPL

Comments are closed.