The House of Favourite Newspapers

Diamond, Kiba, Harmonize Kukiwasha Uzinduzi wa Kampeni za CCM Leo

0
Kutoka kushoto Diamond, Ali Kiba na Harmonize.

Wakali wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond, Ally Kiba, Harmonize wanatarajiwa kukiwasha katika uzinduzi wa Kampeni za CCM zinazotarajiwa kuzinduliwa leo Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Akizungumza na wanahabari wanahabari jijini hapa leo Katibu Itikadi na Uenezi wa Siasa, Humphrey Polepole amesema maandalizi yote ya uzinduzi huo yameshakamilika.

Polepole akielezea uwepo wa wasanii hao na mambo mengine.

Polepole amesema katika kampeni hizo mgombea urais kupitia chama hicho, Dkt. John Pombe Magufuli ataelezea jinsi atakavyoiboresha Tanzania mara tatu zaidi ya aliyoyafanya.

Akizungumzia burudani zitakazopamba uzinduzi huo amesema wasanii wa bongo fleva Diamond, Ali Kiba, Harmonize, Shilole na wengineo zaidi ya mia mbili watapanda jukwaani kutoa burudani.

Sehemu ya wanahabari waliokuwa wakimsikiliza Polepole (hayupo pichani).

Wasanii wa Bongo Muvi nao watapanda jukwaani kunesha kipaji vyao. Alisema Polepole.

Baadhi ya wasanii wa Bongo Muvi waliopo jijini hapa ni pamoja na Johari, Aunty Ezekiel, Asha Boko, Steve Nyerere na wengineo.

Polepole akionesha jukwaa lilivyokamilika.

HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS/GPL, DODOMA

Leave A Reply